Recent Posts

Aliyepika jana na kula jana hajui kesho kama atakula kama alivopika jana au juzi.Aliyeko ugenini hapati picha ya kurudi nyumbani kwani anawasiwasi kama ataweza kuishi kama anavoishi ugenini?Muda wazidi kwenda lakini hajui kama muda wa kwenda bado ajidai katika mawe meupe.

Ajifananisha yeye na ugeni hajui kama yeye atabaki kuwa yeye na mgeni atabaki kuwa mgeni hata kama akikubeba mgongoni.Nashangaa pale mnapolilia nyumbani huku umekaa sebuleni ugenini,wazungumzia sana bara langu wakati wewe jasho lako laishia ugenini.

mganii ashangaa ngozi yako ndugu yangu,haamini kama si ni viumbe kama wao,wakati umefika RUDI NYUMBANI,mgeni anatamani akufukuze lakini anapata faida nawe,yani wewe ni mtaji kwa mgeni.Waona kumbe kuoni,walala kumbe walima,Rudi HOME.

Posted by nyahbingi worrior. Friday, December 24, 2010

3 comments

  1. Simon Kitururu anasema:
  2. Bonge la ujumbe!

     
  3. Anonymous anasema:
  4. Kama kupe na ng'ombe...

     
  5. Mkuu Simon kama ni bonge la sms,umefanya maamuzi?

    Serina Serina kama ni kupe na ng'ombe nani afaidi?

     

Post a Comment

Followers

Popular Posts

Luihamu Ringo