Recent Posts

Msichana wa kiafrika anaweza kufananishwa na ua au mauwa.

Ua linapochanuwa hupendaza na huvutia kwa yoyote yule apitaye karibu au mbali.

Swali...

Mwanaume anaweza kufananishwa kama ua?

Basi...

Kwa dada zangu,mnapendeza sana,mnavutia sana lakini kumbukeni,mnachanua kisha mnanyauka.Kuweni makini na nguo mzivaazo,kuna nguo za kisasa zinatisha,sio tena mini sketi hapana kuna suruali nyepesi ambazo zinaonyesha umbile lenu mvaapo na mpitapo barabarani.

Dada zangu kumbukeni....

Miili yenu ni HEKALU la mfalme.

Pia kumbukeni,utatamanika na utatumika kisha utatoswa jalalani.

Je....

Inafaida gani kuvaa nguo zionyeshazo maumbile yako?

Posted by nyahbingi worrior. Sunday, May 1, 2011

1 Responses to Mauwa mazuri yanameremeta lakini HUNYAUKA.

  1. Simon Kitururu anasema:
  2. Ua zuri kama ni MOYO/Roho ya mtu ,...
    ... labda halinyauki aisee!

    Ingawa nakubali TAKO kama UA hunyauka !:-(

     

Post a Comment

Followers

Popular Posts

Luihamu Ringo