Recent Posts

Unajuwa bwana kuna baadhi ya blogu nikifunguwa napata kichefuchefu,huzuni,majozi.

Nikisoma baadhi ya maoni katika blogu tofauti tofauti nasikitika,nasikitikia Afrika yangu.

Nikiangalia picha katika baadhi ya blogu,nahuzunika sana tena sana.

Katika dunia ya tatu,blogu zetu zinahitaji habari kuhusu MAJEMBE,MBEGU,MASHAMBA,MIMEA,AINA TOFAUTI YA MITI na sio kuhabarisha kuhusu aina ya mavazi au viatu vipya vilivyoingia au kubuniwa.

Nasikitika pale naposoma habari za vilabu vya mpira vya ughaibuni huku tukivisahau vilabu vyetu na wachezaji wetu.

Nafahamu fika silazimishwi kufunguwa blog ambayo itanisikitisha lakini sina budi kwani napenda kujifunza kutoka kwa blogu nyingine lakini post hizo haziendani na maadili ya Mwafrika kimavazi,kielimu n.k.

Inauma sana tena sana unaposoma maoni ambayo hayajengi bali yanabomowa.

Hivi Blog ni nini?

kumbukeni

we were bloggers na blogs of our fathers.

Posted by nyahbingi worrior. Wednesday, February 3, 2010

3 comments

  1. Mija Shija Sayi anasema:
  2. Sipati picha kabsaaaaaaaaaaaaa mkeo atakuwaje Kaka Lui?

     
  3. Unknown anasema:
  4. Nyahbingi: ndiyo kazi ya utandawazi-wizi kwa hiyo usilalame sana. Hata hivo meseji SENT:-(

    Da Mija: yuko as natural as mti ule alokuwa anapumzikia mzee nabii wa kisukuma ng'wanamalundi!!!

    Chacha o'Wambura a.k.a Ng'wanambiti!

     
  5. Da Mija ndio maana mpaka leo sijapata mke au mchumba kwasababu wengi nao kutana nao hawanielewi kabisa.

    Chacha nimekupata mkuu.

     

Post a Comment

Followers

Popular Posts

Luihamu Ringo